Ili kuendeleza zaidi biashara ya vyakula vinavyoagizwa kutoka nje na kuhakikisha usalama wa chakula, General Administration of Customs of China hivi karibuni imerekebisha na kutoa “Kanuni za Jamhuri ya Watu wa China kuhusu Usajili na Usimamizi wa Makampuni ya Uzalishaji ya Nje ya Nchi ya Vyakula Vinavyoagizwa” (Amri Na. 280 ya General Administration of Customs of China) pamoja na tangazo la utekelezaji wake (Tangazo Na. 27 la mwaka 2026 la General Administration of Customs of China). Kanuni hizi mpya zitaanza kutumika tarehe 1 Juni, 2026.
Kanuni zilizorekebishwa zimeundwa kwa umakini ili kuhakikisha zinaendana kwa urahisi na mifumo iliyopo ya usajili. Shughuli za biashara ya vyakula vinavyoagizwa kutoka nje kwa makampuni 96,000 yaliyosajiliwa hazitaathiriwa na kanuni hizi mpya. Kwa mujibu wa takwimu, asilimia 95 ya makampuni yaliyosajiliwa yataweza kufanya upya usajili wao moja kwa moja, huku yale ambayo hayawezi kufanya hivyo sasa yameongezewa muda wa kuwasilisha maombi ya upya usajili kutoka miezi 3–6 kabla ya kumalizika hadi miezi 3–12.
Kwa waombaji wapya, mchakato umerahisishwa kupitia kupunguzwa kwa mahitaji ya nyaraka pamoja na kuanzishwa kwa mfumo wa “Usajili kwa Orodha (List-based Registration)” unaowezesha njia ya haraka ya usajili.
Nyaraka zilizotajwa hapo juu pamoja na maelezo ya ufafanuzi zinapatikana kwa kupakuliwa kupitia tovuti rasmi ya Ofisi ya Usalama wa Chakula cha Uagizaji na Uuzaji Nje ya General Administration of Customs of China(http://jckspj.customs.gov.cn/)).Iwapo kutatokea changamoto yoyote wakati wa mchakato wa usajili wa makampuni, Ubalozi wetu utasaidia kuwasiliana na Ofisi ya Usalama wa Chakula cha Uagizaji na Uuzaji Nje ya General Administration of Customs of China ili kutoa msaada unaohitajika, ikiwemo ushauri na mafunzo.





