Mwanzo > Habari Mpya za ubalozi wa China
Balozi Chen Mingjian: Diplomasia ya China Inafuata Uelekeo Sahihi wa Historia
2022-03-22 16:40

Mnamo Machi 21, makala ya Balozi Chen Mingjian yenye kichwa "Diplomasia ya China Inafuata Uelekeo Sahihi wa Historia" ilichapishwa na magazeti matatu makubwa ya Tanzania, ambayo ni Nipashe, Daily News na The Citizen. Hapa kuna maandishi kamili:

Wakati wa "Mikutano Mikuu Miwili" ya kila mwaka (Bunge la Taifa na Mkutano wa Mashauriano ya Kisiasa ya Watu wa China), Waziri wa Mambo ya Nje wa China anafanya mkutano unaofuatiliwa kwa ukaribu na waandishi wa habari ili kutambulisha sera ya mambo ya nje ya China na maoni na mapendekezo yake kuhusu hali ya kimataifa na masuala yaliyotuta hisia, akitoa tafsiri ya kina ya uhusiano wa China na ulimwengu wa nje.  Tarehe 7 Machi mwaka huu, Mjumbe wa Baraza la Taifa na Waziri wa Mambo ya Nje Wang Yi alifanya mkutano na waandishi wa habari tena na kujibu maswali 27 kutoka kwa vyombo vya habari vya China na vya nje katika muda wa dakika 100, akizungumzia mabadiliko ya sasa ya uhusiano wa kimataifa, na kuelezea kwa uwazi sifa pekee, utume na mwelekeo wa diplomasia ya China.

I. Kudumisha imara amani na maendeleo ya ulimwengu na kulinda usawa na haki kimataifa

Ulimwengu unapitia mabadiliko makubwa ambayo hayajaonekana katika karne moja.  Wakati janga la UVIKO-19 likiendelea kuibuka, mzozo wa Ukraine unaibuka.  Je, China inaweza kuleta utulivu zaidi na nguvu chanya kwa ulimwengu wenye mashaka?  Katika maneno yake yenye ufasaha, Mjumbe wa Baraza la Taifa Wang Yi aliuambia ulimwengu kwamba China itatunza ahadi yake na kutimiza matarajio yake ya awali, kuheshimu ahadi zake, na kuendelea kujenga amani ya dunia, kuchangia maendeleo ya kimataifa na kulinda utaratibu wa kimataifa.

Kuhusu hali ya Ukraine, zingatio la mtizamo wa kimataifa, Mjumbe wa Baraza la Taifa Wang Yi alifafanua kwa mara nyingine msingi wa msimamo wa China, akisema kwamba China itajitegemea katika kutathmini hali hiyo na kutoa msimamo wake kwa misingi ya ustahili wa suala hilo.  Huku akitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuzidisha juhudi za kukuza mazungumzo ya amani, Wang Yi alipendekeza "mpango wa mambo sita" wa China kuhusu kuzuia mgogoro mkubwa wa kibinadamu nchini Ukraine.  Alitangaza kuwa Chama cha Msalaba Mwekundu cha China kitaipatia Ukraine sehemu ya vifaa vya dharura vya kibinadamu haraka iwezekanavyo.

Katika masuala mengine yaliyovuta hisia, Mjumbe wa Baraza la Taifa Wang Yi alitoa wito kwa pande zote zinazohusika kufuata kanuni ya  "Afghan-led and Afghan-owned” kusaidia watu wa Afghanistan katika Kilindi cha matatizo, alisisitiza kuwa uwezo wa kulinda usalama na maendeleo katika Mashariki ya Kati lazima urejeshwe kikamilifu kwa watu katika eneo hilo, na kuzitaka pande zinazohusika kukutana katikati kutafuta suluhu la kisiasa la masuala ya Peninsula ya Korea.  Haya yote yanathibitisha kikamilifu kwamba China, ikiwa ni mjumbe wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na nchi kubwa inayowajibika, daima imekuwa ikishikilia maono ya pamoja, ya kina, ya ushirika na usalama endelevu, na ilichukua jukumu linalofaa katika kulinda amani na utulivu wa dunia.

Mpango wa Ukanda na Njia (BRI) na Mpango wa Maendeleo Ulimwenguni (GDI) ni mipango mikuu ya ushirikiano iliyowekwa na Rais Xi Jinping.  Ni bidhaa muhimu za umma zinazochangiwa na China kwa ajili ya ushirikiano wa maendeleo ya kimataifa.  Hadi sasa, familia ya BRI ina wanachama 180, na GDI imepokelewa kwa shauku na kuungwa mkono na UN na karibu nchi 100.

Mjumbe wa Baraza la Taifa Wang Yi alisisitiza kuwa China itafanya kazi na jumuiya ya kimataifa ili kufikia ushirikiano wa ngazi ya juu, ufanisi bora wa gharama, usambazaji bora wa hali ya juu na ustahimilivu wa maendeleo, ili kuufanya Mpango wa Ukanda na Njia kuwa "ukanda wa maendeleo" kwa manufaa ya  dunia. Alisema China itafanya kazi na pande zote katika maeneo manne ili kutekeleza mpango wa GDI hatua kwa hatua: Kwanza, kuendeleza ushirikiano katika maeneo yaliyopewa kipaumbele;  Pili, kukabiliana na mahitaji ya nchi zote;  Tatu, kushirikiana na taratibu za ushirikiano;  Nne, kuwafikia washirika wa sekta zote.  China itafanya kazi na nchi nyingine zote ili kuhakikisha kwamba hakuna nchi au mtu binafsi anayeachwa nyuma na hakuna matarajio yanayopuuzwa, ili kujenga kwa pamoja jumuiya ya maendeleo ya kimataifa.

Wakati utaratibu wa kimataifa unakabiliwa na changamoto ambazo hazijawahi kushuhudiwa na utawala wa kimataifa unakumbwa na mkanganyiko, tunapaswa kufanya nini?  Jibu lililotolewa na Mjumbe wa Baraza la Taifa Wang Yi ni kuimarisha mshikamano na ushirikiano chini ya bendera ya ushirikiano wa pande nyingi na kujenga kwa pamoja jumuiya yenye mustakabali wa pamoja wa wanadamu. Alisema ni lazima tushikilie msimamo wa pande nyingi, kutetea maadili ya kawaida ya utu, kulinda mfumo wa kimataifa na Umoja wa Mataifa katika msingi wake, kuzingatia kanuni za msingi zinazoongoza mahusiano ya kimataifa kwa kuzingatia madhumuni na misingi ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa, na kufanya kazi kwa ajili ya haki na mfumo wa utawala wenye usawa zaidi duniani.  Ili kuongoza mageuzi ya mfumo wa utawala wa kimataifa na dhana ya usawa na haki, China imekuwa ikisonga mbele kwa ujasiri.

II. Kuimarisha uongozi wa Chama cha Kikomunisti cha China na kulinda kwa uthabiti maslahi ya taifa na furaha ya watu.

Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) ni uti wa mgongo wa watu wa China na nguzo ya diplomasia ya China. Mjumbe wa Baraza la Taifa Wang Yi alisema kuwa kusimulia vizuri hadithi za ustawi wa CPC na kuwasilisha, kutetea na kuendeleza jina zuri la CPC ni kazi muhimu na jukumu muhimu ambalo huduma ya kidiplomasia ya China inapaswa kutekeleza.  Kadiri nchi nyingi zaidi zinavyotumaini kujifunza kuhusu siri” za mafanikio ya CPC, tutaendelea kuwasilisha simulizi za CPC vizuri ili marafiki wengi zaidi wa kimataifa waweze kuelewa CPC, na jumuiya ya kimataifa iweze kuiona CPC kupitia lenzi angavu zaidi.

Akijibu majaribio ya baadhi ya nchi ya kuishambulia China kwa kisingizio cha "kukuza demokrasia", Mjumbe wa Baraza la Taifa Wang Yi alisisitiza kuwa demokrasia ya watu katika mchakato wote wa China ni demokrasia pana, halisi na yenye ufanisi, ambayo inafurahia kuidhinishwa kwa moyo wote na kuungwa mkono na watu wa China pamoja na kutambuliwa kote ulimwenguni. Demokrasia katika nchi tofauti inapaswa kuchanua kama maua tofauti, na kudhani kuwa kuna mfumo mkamilifu usio na makosa sio tu kinyume na ari ya demokrasia, lakini pia inaashiria maafa kwa demokrasia.

"Kuwahudumia watu na kutatua matatizo yao" ni wajibu wa huduma ya kidiplomasia ya China."  Huu ni muhtasari wa kina wa madhumuni na utume wa diplomasia ya China na Mjumbe wa Baraza la Taifa Wang Yi.  Mnamo mwaka 2021, kwa kufuata kanuni inayozingatia watu, China iliandaa shughuli za uokoaji wa dharura baada ya mabadiliko ya ghafla ya hali ya Ukraine, ilitoa chanjo kwa mamilioni ya raia wa China wanaoishi katika nchi 180 dhidi ya UVIKO-19, kushughulikia kesi zaidi ya 60,000 za msaada kwa raia wake wanaoishi nje, na  ilifanikiwa kuokoa makumi ya raia wa China waliotekwa nyara. Mwaka 2022, China itajikita zaidi katika kuunda jukwaa la huduma bora za kibalozi, kujenga mfumo wa ulinzi wa raia wa China na masilahi yao nje ya nchi, na kuzindua mpango wa kuwezesha usafiri salama na usiozuiliwa, ili kulinda maisha na masilahi halali ya Wachina wa ng'ambo.

III.  China itakuwa daima mwanachama wa dunia inayoendelea, na kusimama bega kwa bega na marafiki wa Afrika

China ndiyo nchi kubwa zaidi inayoendelea duniani.  Kuimarisha mshikamano na ushirikiano na idadi kubwa ya nchi zinazoendelea ni chaguo thabiti la kimkakati ambalo China imefanya.  Katika mkutano na waandishi wa habari, Mjumbe wa Bazara la Taifa hilo Wang Yi alijibu maswali ya vyombo vya habari mfululizo kuhusu uhusiano wa China na nchi za ASEAN, nchi za Asia ya Kati, Afrika, Amerika ya Kusini na nchi za visiwa vya Pasifiki ya Kusini.  Majibu yake yametuma ujumbe mzito kwamba China itakuwa daima mwanachama wa nchi zinazoendelea na mshirika wa dhati na wa kutegemewa wa nchi zinazoendelea.  Mwaka huu, China itachukua uenyekiti wa BRICS kama fursa ya kuunganisha zaidi sauti na nguvu za masoko yanayoibukia na nchi zinazoendelea, na kusaidia kufanya utaratibu wa kimataifa kuwa wa haki na usawa.

Mahusiano kati ya China na Afrika daima yamo katika ajenda ya mkutano na waandishi wa habari wa Waziri wa Mambo ya Nje wa China wakati wa "Mikutano Mikuu Miwili" ya kila mwaka.  Hii inaonyesha kikamilifu umuhimu wa uhusiano kati ya China na Afrika katika diplomasia ya China. Mjumbe wa Baraza la Taifa Wang Yi alisema kuwa kwa miaka mingi, China imejenga zaidi ya kilomita 10,000 za reli, hadi kilomita 100,000 za barabara kuu, karibu bandari 100, na hospitali na shule zisizohesabika - Afrika, akisisitiza kwamba hii sio "mitego ya madeni"  bali alama ya ushirikiano.  Akibainisha kuwa mwaka huu China na nchi za Afrika zimeanza kutekeleza yale yaliyotolewa na Mkutano wa Nane wa Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC), Wang Yi alisema kuwa China itaheshimu ahadi yake ya kushirikiana na Afrika, kutetea ari ya urafiki wa China na Afrika na ushirikiano, na kufanya kazi na mataifa ya Afrika kutekeleza "programu tisa" za ushirikiano na Afrika zilizotangazwa na Rais Xi Jinping.

Mjumbe wa Baraza la Taifa Wang Yi alipendekeza vipaumbele vitatu vya ushirikiano wa China na Afrika mwaka huu.  Kwanza, China itaendeleza kwa nguvu ushirikiano wa kupambana na UVIKO na Afrika, kutimiza kikamilifu ahadi ya Rais Xi Jinping ya kutoa dozi bilioni moja za chanjo kwa bara hilo, na kuisaidia Afrika kuongeza uwezo wa uzalishaji wa chanjo barani humo.  Pili, China itaunganisha GDI na Ajenda 2063 ya Umoja wa Afrika na kuchukua hatua madhubuti kusaidia ufufuaji wa uchumi na maendeleo endelevu ya Afrika. Tatu, China itachukua hatua kuhusu Matazamio ya Amani na Maendeleo katika Pembe ya Afrika, na kuchukua jukumu muhimu kwa ajili ya amani na maendeleo ya Pembe ya Afrika na Bara la Afrika kwa ujumla.

Suggset To Friend:   
Print