Balozi Chen Mingjian Ahudhuria Saluni Maalum ya Kitamaduni - Balladi za Wuxi: Taswira ya Mji wa Maji
2025-05-21 23:57
Mei 15, Ubalozi wa China nchini Tanzania uliandaa “Saluni maalum ya Kitamaduni - Balladi za Wuxi: Taswira ya Mji wa Maji”. Mhe. Balozi Chen Mingjian, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mbunge), wajumbe wa Jumuiya ya Kidiplomasia, na wawakilishi wa Tanzania katika sekta ya utamaduni na vyombo vya habari walihudhuria hafla hiyo.

Wageni walifurahia tamthiliya bora ya Kikundi cha Wuxi Pingtan, na kujipoteza kwenye milio ya kuvutia ya simulizi za kitamaduni za Kichina. Pia walifurahia maonyesho ya uandishi wa maandishi na sanaa ya chai, wakijionea uzuri wa sanaa na utamaduni wa Kichina.
