Mwanzo > Habari Mpya za ubalozi wa China
Vijana wa Kitanzania Waalikwa Kutazama Hafla ya “Ongea na Wanaanga” Mtandaoni na Kurekodi Video za Maswali
2022-07-09 03:40

Kuzunguka katika mbingu kubwa ili kuchunguza anga ya kushangaza ni matarajio ya kawaida ya wanadamu. Mnamo Juni 5, 2022, chombo cha anga za juu cha China cha Shenzhou-14 kilizinduliwa kwa mafanikio, na kutuma kwenye kituo cha anga cha Tiangong wanaanga watatu, ambao ni Chen Dong, Liu Yang na Cai Xuzhe, ambao walipaswa kutumia miezi sita angani. 

Ujumbe wa China kwenye Umoja wa Afrika, Shirika la Anga za Juu la China, na Umoja wa Afrika zitashirikiana kuandaa hafla ya "Ongea na Wanaanga" mwishoni mwa Agosti, na kuwaalika vijana wa Afrika kufanya mazungumzo na wajumbe watatu wa China kuhusu mada zinazowavutia.

Ubalozi wa China nchini Tanzania unawaalika vijana wa Kitanzania kutazama mubashara hafla ya "Ongea na Wanaanga" mtandaoni, ili kupata ufahamu bora wa maisha ya wanaanga angani na kuchochea shauku ya uchunguzi wa anga kwa kusikiliza simulizi za wanaanga wa China juu ya uzoefu wao katika anga na ubunifu mkubwa wa kisayansi na kiteknolojia wa chombo cha anga za juu Shenzhou-14. 

Kabla ya hafla hiyo, tunawaalika marafiki vijana wa Kitanzania kuandika mada na maswali wanayotaka kuwasiliana nao na kuwauliza wanaanga hao watatu wa Kichina katika lugha ya Kiingereza au Kichina, na kurekodi video fupi au kupiga picha unapowasilisha mada na maswali. Vijana wa Kitanzania wanaombwa kutuma video na picha zao kwa anwani zifuatazo kabla ya Julai 17: mfa_fzsltb@163.com; chinaemb_tz@mfa.gov.cn

Waandalizi wa hafla hiyo watachagua na kuhariri video na picha zilizopokelewa, na kutangaza baadhi yao wakati wa hafla hiyo. Aidha, Ubalozi huu pia utachagua baadhi ya video na picha za kuchapisha kwenye tovuti ya ubalozi na majukwaa ya vyombo vya habari vya ndani. Watayarishaji hao ambao video au picha zao zimechaguliwa watapokea nyenzo za kutia moyo kutoka kwetu. 

Tunatazamia ushiriki wenu hai, marafiki vijana wa Tanzania!        

                     

                                                    Ubalozi wa China nchini Tanzania

                                                                Julai 8, 2022   


Suggset To Friend:   
Print